Halloween party ideas 2015

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto UMMY MWALIM amesema serikali imeagiza chanjo kutoka shirika la kimataifa la kuhudumia watoto
Shirika  la kuhudumia watoto duniaani UNICEF
.


Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto UMMY MWALIM amesema serikali imeagiza chanjo kutoka shirika la kimataifa la kuhudumia watoto UNICEF na kuongeza kuwa tayari HAZINA imetoa zaidi ya shilingi Bilioni 6.4 kwa ajili ya kukabiliana na tatizo hilo.



Waziri UMMY amewambia waandishi wa habari mjini DODOMA kuwa baadhi ya chanjo zinatarajiwa kuwasili baadaye mwezi huu na kusambazwa kwenye vituo vyote vya afya  nchini.
Waziri UMMY amesema kuwa sio maeneo yote yenye upungufu wa chanjo, hivyo amewaagiza waganga wakuu wa mikoa kukusanya na kutoa takwimu za upungufu huo.

September 16,2016

TANZANIA inakabiliwa na uhaba wa wataalamu wenye ujuzi wa kufanya matengenezo ya vifaa vya maabara, hali inayodaiwa kudhoofisha
 
TANZANIA inakabiliwa na uhaba wa wataalamu  wenye ujuzi wa kufanya matengenezo ya vifaa vya maabara,  hali  inayodaiwa kudhoofisha utoaji wa vipimo mbalimbali kwa wagonjwa.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa mkutano wa Wakaguzi  wa Maabara Binafsi kutoka mikoa yote nchini  unaofanyika  mkoani SINGIDA.

Akifungua Mkutano huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakaguzi wa Maabara Nchini Dakta MARGARET  MHANDO amesema kuwa mpaka sasa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wizara ina wataalamu watatu wa aina hiyo ambao hawakidhi mahitaji katika hospitali zilizopo hapa nchini.

Dakta MHANDO amewataka Wakaguzi  wa Maabara Binafsi kutoka mikoa yote nchini  kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa mara kwa mara wa maabara zote zilizopo nchini ili kuhakikisha maabara hizo zinatoa huduma na vipimo sahihi kwa wagonjwa.

 September 15, 2016
LEONARD MANGA
 == =

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU amesema kuwa Wizara yake itaanzisha mpango wa Taifa
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU amesema  kuwa Wizara yake itaanzisha mpango wa Taifa wa kupima Saratani ya Shingo ya Uzazi na Matiti kwa Wanawake wote nchini.

Waziri UMMY MWALIMU amesema kuwa mpango huo unalenga kupunguza wagonjwa wanaofikishwa katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road iliyopo Jijini DSM wakiwa katika hatua za mwisho.
       
Waziri huyo wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ametoa kauli hiyo mkoani DODOMA wakati wa mafunzo ya Usimamizi na Udadisi wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi hapa nchini.


September 15, 2016
IDD MAALIM
 == =

Kwa muda mrefu huduma ya upasuaji nchini Tanzania imekuwa ikitumia mbinu zinazo walazimu madaktari kumpasua mgonjwa katika baadhi ya maeneo ya mwilini kwa mjibu wa utalaamu wa kitabibu hali ambayo husababisha majeraha na maumivu ya eneo lililopasuliwa.Image result for Upasuaji usio na maumivu waanza Tanzania
Na sasa mfumo mpya wa upasuaji umeanza,ambapo hakuna ulazima wa kumpasua tena mgonjwa bali hupewa huduma hiyo kupitia vijitundu vidogo tofauti na mfumo wa zamani hali inayopunguza maumivu na maambukizi .Image result for Upasuaji usio na maumivu waanza Tanzania
Mwandishi wa BBC Halima Nyanza ameshuhudia aina hiyo mpya ya upasuaji na kutuandalia taarifa ifuatayo.Image result for Upasuaji usio na maumivu waanza Tanzania

Wachunguzi wa masuala ya mazingira nchini Urusi wanajaribu kubaini sababu iliyoyafanya maji ya mto ulio karibu na kiwanda cha nikeli cha kampuni ya Norilsk Nickel kubadilika na kuwa ya rangi nyekundu.

Picha za maji ya mto Daldykan ambayo yamebadilika rangi zimesambazwa sana katika vyombo vya habari Urusi.

Gazeti la serikali la Rossiiskaya Gazeta linasema kuvuja kwa bomba la kusafirisha taka za mchanganyiko wa shaba nyekundu na nikeli huenda likawa kiini cha maji hayo kubadilika rangi.

Norilsk Nickel ndiyo mzalishaji mkubwa zaidi wa nikeli na palladium duniani.Zvezda TV


Kampuni hiyo ina vinu na tanuri nyingi rasi ya Taimyr eneo la Krasnoyarsk katika jimbo la Siberia. Ujenzi wa vinu hivyo vikubwa ulifanyika enzi za muungano wa Usovieti.

Kampuni hiyo ina kiwanda kwa jina Nadezhda karibu na mto Daldykan lakini maafisa wake wanasema hawajapata dalili zozote za uchafuzi kutoka kwa kiwanda hicho.

Rais wa kampuni hiyo ni bilionea Vladimir Potanin.

Habari za kutokea tetemeko ya ardhi mikoa ya Kagera,Mwanza na mara.

Ripoti za awali zimesema tetemeko hilo lenye kipimo cha Richter 5.7 limeharibu nyumba nyingi mkoani Kagera.

Majengo kadha yanaripotiwa kuharibiwa katika miji iliyo karibu.
Hata hivyo hakuna taarifa zaidi za kuwepo maafa . Mitetemeko mingine midogo pia ilisikika katika mataifa jirani ya Kenya na Rwanda.

Tutawajuza jinsi habari zaidi zitakavyokuwazinapatikana.

Shirika la Afya Duniani WHO limeonya kwamba watu wanaotoka katika maeneo ambayo yana maambukizi na kusambaa kwa ugonjwa wa ZIKA

Shirika la Afya Duniani WHO limeonya kwamba watu  wanaotoka katika maeneo ambayo yana maambukizi na kusambaa kwa ugonjwa wa ZIKA wanapaswa kujihusisha mahusiano salama ya ndoa wenzi wao katika kipindi cha miezi sita ili kuzuia uwezekano wa kusambaa kwa ugongwa huo.

ZIKA ni ugonjwa ambao unasambazwa na mbu husababisha watoto kuzaliwa na vichwa vidogo.
Ugonjwa huo huambukizwa kwa binanadumu kupitia maji maji ya mwili hivyo wataalamu wa afya wanaonya kwamba watu hasa wapenzi wanaotoka katika maeneo yenye maambukizi ya ZIKA kuchukua tahadhari ya kuambukizana ugonjwa huo.

September 7, 2016
MBOZI KATALA

Baadhi ya hospitali jijini DSM hazina baadhi ya chanjo hali iliyowafanya watumishi wa hospitali na wagonjwa kuiomba serikali kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo

Wakizungumza na TBC wamesema kukosekana kwa chanjo hizo ikiwemo ya pepopunda kunaweza kusababisha vifo na ulemavu usiotarajiwa hususan kwa wajawazito, watoto wachanga na majeruhi wa ajali.

Taarifa za kukosekana kwa baadhi ya chanjo katika hospitali mbalimbali jijini DSM zikiwemo zile zinazotumiwa na wajawazito zimeifanya TBC kutembelea baadhi ya hospitali jijini humo ikiwemo Hospitali ya MNAZI MMOJA ili kufahamu hali halisi.

JANETH SUDA ni Muuguzi wa Afya ya Jamii, Mama, Baba na Mtoto katika Hospitali ya MNAZI MMOJA ambaye amesema chanjo ya tetenasi au pepo punda haipo katika hospitali hiyo.

Daktari kiongozi Hospitali ya Rufaa ya Amana STANLEY BINAGI ameonesha wasiwasi wa madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukosefu wa chanjo hizo muhimu kwa binadamu.

Kupata ufafanuzi wa jitihada zinazofanywa na serikali kukabiliana na upungufu wa chanjo mwandishi wa TBC EDWARD KONDELA amezungumza na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Dkt. NEEMA RUSIMABAYILA ambaye amesema serikali imeagiza baadhi ya chanjo ikiwemo ya tetenasi au pepo punda zinazotarajiwa kufika kuanzia tarehe 19 mwezi huu, ambazo zitaweza kutumika kwa muda wa miezi mitatu.

September 9, 2016
 EDWARD KONDELA

Wazee wamelalamikia kutojumuhishwa katika mipango endelevu ya kitaifa SDG na kushindwa kupata mikopo katika mabenki , bima na mifuko ya vikoba kutokana na kuonekana hawafai kiuchumi

Wakizungumza wakati wa semina ya kuwashirikisha wazee kwenye malengo ya millennia iliyoandaliwa na taasisi ya utafiti wa kiuchumi na kijamii ESRF na HELPAGE baadhi ya wazee hao wamesema pamoja na kupewa pensheni lakini fedha hizo hazitoshi kuanzisha mradi wowote wa maendeleo na kuwafanya kuwa masikini.

Kwa upande wake Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto UMMY MWALIMU amesema serikali imeanza kuwaondolea changamoto zote wazee kwa kuwaongezea kipato kwa kuwapa pensheni wazee wote, huduma za afya bure na wanatarajia kuanzisha mfuko wa wazee

 September 1, 2016

Dodoma. Wanajeshi wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) wamechangia chupa 30 za damu katika kituo cha damu salama Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Jumla ya maofisa 60 waliofnya zoezi la usafi na kuchangia damu ikiwa ni miongoni mwa shughuli za kusherehekea maadhimisho ya miaka 52 ya jeshi hilo.
JWTZ KUCHANGIA DAMU

Kamanda mkuu wakanda ya kati Brigedia Jenerali Masumbuko Mademe alisema jana kuwa wameamua kusherehekea siku iyo kwa kuchangia damu baada ya kupata taarifa  kuwa mkoa waDodoma kuna upungufu wa damu.

Pamoja na kuwalinda wananchi na mali zao tumeguswa tatizo la uhaba wa damu salama Dodoma tumeona ni vema sisi kuonyesha mfano wa kuchangia damu salama
Mganga mkuu wa mkoa wa Dodoma. Dk Charles kilogwe aliwaomba wakazi wa mkoa huo na taasisi nyingine za serikali kiuga mfano huo ili kunusuru maisha ya watanzania wanaopteza maisha kwa kukosa
damu.

Alisema mahitaji ya damu salama mkoani hapa lit 200 na kwamba wamekuwa wakikusanya lita 150.
Powered by Blogger.