Halloween party ideas 2015

TANZANIA inakabiliwa na uhaba wa wataalamu wenye ujuzi wa kufanya matengenezo ya vifaa vya maabara, hali inayodaiwa kudhoofisha
 
TANZANIA inakabiliwa na uhaba wa wataalamu  wenye ujuzi wa kufanya matengenezo ya vifaa vya maabara,  hali  inayodaiwa kudhoofisha utoaji wa vipimo mbalimbali kwa wagonjwa.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa mkutano wa Wakaguzi  wa Maabara Binafsi kutoka mikoa yote nchini  unaofanyika  mkoani SINGIDA.

Akifungua Mkutano huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakaguzi wa Maabara Nchini Dakta MARGARET  MHANDO amesema kuwa mpaka sasa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wizara ina wataalamu watatu wa aina hiyo ambao hawakidhi mahitaji katika hospitali zilizopo hapa nchini.

Dakta MHANDO amewataka Wakaguzi  wa Maabara Binafsi kutoka mikoa yote nchini  kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa mara kwa mara wa maabara zote zilizopo nchini ili kuhakikisha maabara hizo zinatoa huduma na vipimo sahihi kwa wagonjwa.

 September 15, 2016
LEONARD MANGA
 == =

Post a Comment

Powered by Blogger.