Halloween party ideas 2015

Serikali imekanusha taarifa za kuwepo kwa ugonjwa wa HOMA YA ZIKA nchini


Akizungumza na waandishi wa habari jijini DSM, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU amesema  ugonjwa wa homa ya ZIKA bado haujathibitishwa kuingia nchini na kuwatoa hofu wananchi ya uwepo wa ugonjwa huo hapa nchini.

Waziri MWALIMU amesema utafiti uliofanywa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu - NIMR ulikuwa ni utafiti uliofanyika nchini kuchunguza ubora wa kipimo kipya cha kupima magonjwa ya zika na chikungunya ili kujua ubora wa  kipimo hicho.

Post a Comment

Powered by Blogger.