Halloween party ideas 2015

Mganga Mkuu wa Serikali Profesa MUHAMMED KAMBI ametoa wito kwa Wanasayansi nchini kujiridhisha katika tafiti zao na kutoa taarifa ambazo zitakuwa na lugha rahisi inayoeleweka kwa jamii
.
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa MUHAMMED KAMBI ametoa wito kwa Wanasayansi nchini kujiridhisha katika tafiti zao na kutoa taarifa ambazo zitakuwa na lugha rahisi inayoeleweka kwa jamii.

Profesa KAMBI  ametoa wito huo Jijini DSM baada ya kushiriki matembezi na uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza.

Profesa KAMBI pia amesisitiza kuwa kwa sasa hakuna Homa ya ZIKA nchini na kuwataka wanasayansi nchini kufuata taratibu zilizopo wakati wa kutangaza matokeo ya tafiti zao.

Mgeni rasmi katika matembezi na uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza alikuwa ni Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ambaye ametoa muda wa miezi Mitatu kwa halmashauri zote nchini kurudisha serikalini maeneo ya michezo yaliyovamiwa na watu mbalimbali.

Makamu wa Rais  pia amewaagiza viongozi wa mikoa na wilaya zote nchini kuweka utaratibu wa kufanya mazoezi angalau kwa mwezi mara Moja na kutangaza kuwa kila Jumamosi ya pili ya mwezi itakuwa ni siku ya mazoezi.

Kwa uapande wake Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili ALHAJ ALI HASSAN MWINYI ametoa wito kwa Watanzania kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao.

Post a Comment

Powered by Blogger.