Halloween party ideas 2015

Dodoma. Wanajeshi wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) wamechangia chupa 30 za damu katika kituo cha damu salama Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Jumla ya maofisa 60 waliofnya zoezi la usafi na kuchangia damu ikiwa ni miongoni mwa shughuli za kusherehekea maadhimisho ya miaka 52 ya jeshi hilo.
JWTZ KUCHANGIA DAMU

Kamanda mkuu wakanda ya kati Brigedia Jenerali Masumbuko Mademe alisema jana kuwa wameamua kusherehekea siku iyo kwa kuchangia damu baada ya kupata taarifa  kuwa mkoa waDodoma kuna upungufu wa damu.

Pamoja na kuwalinda wananchi na mali zao tumeguswa tatizo la uhaba wa damu salama Dodoma tumeona ni vema sisi kuonyesha mfano wa kuchangia damu salama
Mganga mkuu wa mkoa wa Dodoma. Dk Charles kilogwe aliwaomba wakazi wa mkoa huo na taasisi nyingine za serikali kiuga mfano huo ili kunusuru maisha ya watanzania wanaopteza maisha kwa kukosa
damu.

Alisema mahitaji ya damu salama mkoani hapa lit 200 na kwamba wamekuwa wakikusanya lita 150.

Post a Comment

Powered by Blogger.