Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU amesema kuwa Wizara yake itaanzisha mpango wa Taifa
 |
| Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto UMMY MWALIMU |
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
UMMY MWALIMU amesema kuwa Wizara yake itaanzisha mpango wa Taifa wa
kupima Saratani ya Shingo ya Uzazi na Matiti kwa Wanawake wote nchini.
Waziri UMMY MWALIMU amesema kuwa mpango huo unalenga kupunguza
wagonjwa wanaofikishwa katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road iliyopo
Jijini DSM wakiwa katika hatua za mwisho.
Waziri huyo wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
ametoa kauli hiyo mkoani DODOMA wakati wa mafunzo ya Usimamizi na
Udadisi wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi hapa nchini.
September 15, 2016
IDD MAALIM
== =