MUSWADA WA WAZEE KUPELEKWA BUNGENI
Ummy Mwalimu kwenye maadhimisho ya siku ya wazee duniani ambayo kitaifa yamefanyika wilayani Mbarali mkoani Mbeya. Katika hatua nyingine waziri Ummy Mwalimu ametoa miezi mitatu kwa wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuwatambua wazee wote kwenye maeneo yao na kuwapatia vitambulisho vya matibabu bure ikiwa ni utekelezaji wa sera ya serikali na ilani ya chama cha mapinduzi inayoelekeza wazee nchini kupewa matibabu bure. Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amesema hadi kufikia mwezi juni mwaka huu, zaidi ya asilimia 78 ya wazee waliotambuliwa mkoani Mbeya walikuwa tayari wamepewa vitambulisho kwa ajili ya kupatiwa bure. Mfuko wa taifa wa bima ya afya ni miongoni mwa taasisi zinazotoa huduma ya matibabu kwa wazee ambao pia unao wajibu wa kuhakikisha wazee wanapatiwa matibabu ya bure
Post a Comment