Mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya ziwa imeteketeza kwa moto bidhaa mbalimbali ambazo
haziruhusiwi kutumia na binadamu vikiwemo vyakula na vipodozi, ambavyo vimekamatwa katika oparesheni
kali katika manispaa ya Musoma mkoani Mara baada ya kuingizwa nchini bila kuzingatia utaratibu.
Akizungumza wakati bidhaa hizo zikitekezwa katika dampo la halmashauri ya manispaa ya Musoma eneo la
Buhare, mkaguzi mwandamizi wa TFDA Bw Julius Panga, amesema bidhaa hizo ambazo zimeteketezwa zimo
ambazo hazijasajiliwa hapa nchini, ambazo zinadaiwa kuingizwa kwa njia za panya kupitia mpaka wa Tanzania
na Kenya eneo la Sirari.
Nao baadhi ya maafisa afya wa halmashauri ya manispaa ya Musoma, wakizungumza wakati zoezi la
uteketezaji wa bidhaa hizo likiendelea, wamewaonya wafanyabiashara wanaoingizi dawa na vyakula ambavyo
haviruhusiwi kutumiwa na binadam hapa nchini.
Post a Comment